Wednesday, February 11, 2015

BARCELONA YAMMEZEA MATE ALEXI SANCHEZ WA ARSENAL.

ad300
Advertisement
Barcelona yammezea mate mchezaji Alexi sanchez wa Arsenal
Afisa mpya anayesimamia maswala ya uhamisho wa wachezaji katika kilabu ya Barcelona amesema kuwa ana hamu ya kumsajili tena mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez.
Sanchez aliuziwa Arsenal katika msimu wa kiangazi kwa kitita cha takriban pauni millioni 30 na hadi wakati huo ameonyesha umahiri wake katika ligi ya Uingereza.
Barcelona kwa sasa inahudumia marufuku ya kutosajili ambayo inaendelea hadi mwishoni mwa msimu huu,hatua inayomaanisha kwamba haiwezi kusajili mchezaji mwengine yeyote.
Sanchez amefunga mabao 18 katika mechi 32 na majarida ya michezo nchini Uhispania yameshtumu hatua ya Barcelona kumwachilia mchezaji huo.
Lakini katika mwelekeo mpya ,afisa mpya anayehusika na maswala ya uhamisho wa wachezaji Ariedo Braida amesema angetaka kumsajili tena Sanchez ili kurudi katika uga wa Nou Camp.

 
Mchezaji Alexi Sanchez
''Ningependa kumsajili Sancheza katika kilabu yoyote niliopo''.
''Namjua sana lakini sijui ni sababu gani zilizosababisha kilabu hii kumwachilia,na sasa mchezaji huyo ni miongoni mwa wachezaji wazuri katika ligi ya Uingereza na ari yake iko juu''.
Tayari Arsenal inadaiwa kutafuta sahihi ya Sanchez ili kumuweka katika kilabu hiyo kwa mda mrefu zaidi.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 Post a Comment: