Friday, February 13, 2015

COSTA:SIJAWAHI JERUHI MCHEZAJI

ad300
Advertisement
 
Mshambuliaji wa Chelsea,Diego Costa amaliza kutumikia adhabu
Mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Diego Costa amesema hajawahi kumjeruhi mchezaji mwenzake kwa makusudi mchezoni na kwamba tuhuma hizo dhidi yake ni changamoto anazozipitia na ataendelea kuwa imara. Mchezaji huyo raia wa Brazil mwenye miaka 26 amemaliza kutumikia adhabu ya kutocheza mechi tatu kutokana na kufungiwa kwa kile kilichodaiwa kumuumiza mchezaji wa Liverpool katika mchezo wa nusu fainal mwezi jana. Costa mwenyewe amesema kuwa kuwa hana historia ya mchezo huo mchafu wa kuweza kumuumiza mchezaji mwenzake kwa kudhamiria.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amelalamikia hatua ya kufungiwa kwa mchezaji wake na kudai kuwa ilikuwa ni tukio la bahati mbaya japo amevituhumu vyombo vya habari kwa kulipa uzito mkubwa Zaidi suala hilo kuliko hali halisi.
Costaaliyejiunga na Chelsea kwa paundi milioni 32 mwezi July mwakajana anasema kuwa amekuwa akichezewa vibaya zaidi na wachezaji wengine matukio yanayowastahili kuchukuliwa adhabu kali kwa makosa kama hayo lakini kwake yeye mambo yanakuwa makubwa zaidi.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 Post a Comment: